![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhIES1ZtlvIInNhWX568L-ipDKPpAa9k_sdSke2XwKix1OzZU2SuhKfwCrWTxbGIhGpYu7vQmgCah-ZIr9T-kDPcCVwjtCHq5SRzoX_rjAMTBnpYPXwamHULQ27dyv8-bbnj9xVwktrx1hW/s400/large_Ginger+taangawizi.jpg)
Kwa ujumla tangawizi hustawi kwenye mwinuko kuanzia m 800 mpaka 1500
kutoka usawa wa bahari, kwa ujumla maeneo mengi inakostawi kahawa na
tangawizi zinastawi.
![]() |
Maandalizi ya mwanzo ya shamba kwaajili ya kilimo cha Tangawizi |
KUANDAA SHAMBA
Andaa Shamba lako mapema, katua/lima kuanzia miezi ya
April,
may au June, ni vizuri ukaanzisha Shamba jipya au lilikaa bila kulimwa
kwa miaka mitatu, Lainisha udongo miezi ya August au September na
kuanzia November unaweza kuanza kupanda..
KUPANDA
Tangawizi hupandwa kwa kuivunja vunja kwa kufuatisha mbingili zake.
Panda tangawizi kwa cm 30 kati ya shina moja na jingine na cm 45 mpaka 60
kati ya mstari mmoja na mwingine. Tumia mbolea ya mboji au samadi na
usitumie mbolea za kemikali kupandia, Kg 1000 za tangawizi hupandwa
katika hekta moja na unaweza kuvuna kuanzia tani 10 mpaka 25 inategemea
ukubwa wa mbegu, urutubishaji, kiasi cha maji na palizi. Huchukua wiki
mbili mpaka mwezi mmoja na nusu tangawizi Kuota. Inategemea kiasi cha maji na
joto kwenye udongo, ni vizuri kuzitandaza tangawizi kwenye kivuli na
kufunika na gunia na kuzimwagilia ili ziote kabla hujazikatakata kwa ajili
ya kwenda kupanda. Palilia Mara tu Majani yanapoota na pandishia udongo
kwenye mashina ili tangawizi itanuke vizuri.
MAGONJWA
Tangawizi haishambuliwi sana na magonjwa ila Mara chache hushambuliwa na kuvu (fungus).
KUVUNA
Huchukua miezi 6 mpaka 18 kukomaa, inategemea mwinuko toka usawa wa bahari na mvua.
Tangawizi haitaki maji yanayotuama kama vijaruba vya mpunga, maji
yakituama kwenye shina la tangawizi kwa mda Fulani Majani ya tangawizi
huwa ya njano na huanza kunyauka.
Kuvuna Tani 10 kwa hekta moja ni kadirio la chini kabisa.. Kipindi soko
linapokua zuri unaweza kupata kuanzia Mil 20 mpaka 60 kwa hekta moja,
kuna wahindi ambao hununua tangawizi kwa wingi sana na wanaexport,
wahindi hununua kg 1 kwa sh 3000, mpaka 3500 ukiuzia shambani
Uzuri tangawizi unaweza kusubiri soko zuri na ukauza kwa bei nzuri kwani zao hili hupanda bei haraka.
Watu wengi wanashindwa kuzalisha tangawizi kwa wingi kwa kukosa mitaji
ya kununulia mbegu kwani mbegu zake ni gharama, hivyo unashauriwa
kununua kg chache walau kg 200 ukapanda eneo dogo ili kuzĂ lisha mbegu
ambazo utaweza kuzisambaza eneo kubwa, na kwa kulima eneo dogo unaweza
kupata uzoefu kupitia hapo na kujua kama eneo ulilolima ni sahihi na
linafaa kwa kilimo cha tangawizi.
Sokoni tangawizi huuzwa sh 5000 mpaka 6000 kwa kg soko linapokua zuri, pia tangawizi kuna msimu hushuka bei mpaka sh 2000 kwa kg. Usikatishe tamaa pale tangwizi inaposhuka bei mpaka sh. 1500, unaweza
kusubiri kwa mda mfupi na kuuza tangawizi kwa bei nzuri sana kwa kuwa bei
yake hupanda kwa haraka.
![]() |
Mkulima wa Tangawizi Songea |
HALI YA HEWA
Mimea hii husitawi katika maeneo yenye joto la wasitani yaani haihimili
hali ya joto kali sana,baridi kali, mvua nyingi na udongo unaotuamisha
maji, magonjwa ya fangasi na wadudu waharibifu. Tangawizi hukua vizuri
katika maeneo yenye joto la wastani wa nyuzi kati ya 21-30 sentigradi.
Iwapo Tangawizi itapandwa katika maeneo yenye joto chini ya nyuzi 15 za
sentigrade huchelewa kuota.
MVUA
Kwa upande wa mvua Tangawizi huhitaji kiasi cha mvua kati ya
millimita 400-600 kwa msimu. Mvua nyingi husababisha uwepo wa magonjwa
ya fungusi na bakiteria ambayo huathili mavuno.
HALI YA UDONGO
Huhitaji udongo wenye rutuba nzuri ulio na virutubisho. Vile vile
haihitaji udongo wenye kiasi kikubwa cha tindikali na alikali
kubwa. Hali ya udongo katika kipimo cha pH iwe kati ya 6.0 na 7.0. Ingawa mmea una uwezo vile vile wa kuhimili kwenye udongo wenye pH 5.0.
MAKALA HII IMEANDALIWA NA MTAALAM NA MSHAURI WA MASUALA YA KILIMO,
KINOJA MAPIGANO,
+255768449499 , +255716964704
S.L.P 5960 DSM.
kilimobiashara@gmail.com
habari, natafuta soko kubwa la tangawizi.
ReplyDeleteKil0 bei gani
Delete